Ads 468x60px

Pages

Monday, December 28, 2009

CLIMBING THE MOUNTAIN IN HIGH SPEED......


After years of war they are ready to take a step forward are we ready............

ARE WE THERE YET..................


I believe for every educated Tanzanian must feel responsible to rectify the standard of living of our people.We must take action by investing our skills and potential in ensuring the better living standard for every Tanzania.Better infrastructure comes from an engineer but not just an engineer but the one who is committed to serve his/her country.The same thing goes to politicians,doctors,lecturers and different professionals in our societies,the period of blaming each other is over let do something for our country and stop nonsense politics..............

YANGA MABINGWA WAPYA WA TUSKER.


Young Africans captain Abdi Kassim receives the Tusker Cup from the Minister for Information,Culture and Sports George Mkuchika after his team had beaten Kenya’s Sofapaka 2-1 in the final at the Uhuru Stadium in Dar es Salaam today. Looking on is the President of the Tanzania Football Federation (TFF) Leodegar Tenga.

SIMPLE REALITY..............

Simple reality…………….
My fellow Tanzanians students who are living in Bangalore I woke up this morning and I was encouraged
To tell u something which I think it is very important to understand .Today we are facing a lot of challenges in a job market, especially at this time when government is sending people to study all over the world. I believe at the time we are graduating there will be a lot of people looking for jobs in Tanzania for example people from Russia Turkey, China and Algeria who are studying over there by using the government loan.
What am trying to tell you is that please let us try to use the opportunity we have of studying in a country where by the cost of studying and living is low to do something which will help us to challenge the job market with good potential and skills .In India it is easy to study a lot of additional courses ,since they are cheap compared to other countries and the other good thing is that we are not working we are only studying so I believe we have enough time to do so.
I will take this chance to give you a simple example ,for people who are in the field of computer science they will understand me better .To study CCNA in India is approximately 130usd excluding exam charge while to study the same course in Dar es Salaam is 600usd or more excluding exam charges.
You might complain and say , but those opportunity are available for people in Computer field only .That is not true since there is a lot of courses for people of business and economic fields also courses like Chattered accountants and MIS(management information system) are there waiting for you guys.
For people in the field of Arts and law courses there are lot of seminars and conferences waiting for you to attend.My advice is let us be committed in our education responsibilities because other activities they are not the main goal for us to be here.
If you understand me use this opportunity and you will remember me one day…………………..
posted by
Jumanne R Mtambalike.

TANGAZO LA UBALOZI


Ministry of Foreign Affairs of Tanzania


If you have any information about the custom requirements of Tanzania that could be helpful to others, please use this form to post your comments. Any details related to the customs procedures, regulations, or any other specifics about the customs requirements of Tanzania that will help, we will be greatly appreciated.
Embassy Of Tanzania in India
EP 15, Block C, Chanakyapuri,
New Delhi, 110021
India Phone: +91-11-24122865

Friday, December 18, 2009

WHO IS NEXT ON THE HOT SEAT?

TASABA PRESENT'S

Monday, December 14, 2009

SALAMU ZA KUFUNGA MWAKA ZA MWESHIMIWA RAIS

TANZANIA STUDENTS ASSOCIATION BANGALORE
(TASABA)



14/12/09

Salamu kwenu nyote,

Ndugu wa Tanzania wenzangu napenda kuchukua nafasi hii kuwa kumbusha juu ya swala la kujiandikisha kuwa mwanachama hai wa TASABA. Fomu zote na maelekezo wanayo viongozi wote wa vitongoji. Ni muhimu sana kujiandikisha kwani tunahitaji kujua hapa Bangalore kuna wa Tanzania wangapi pia tuweze kutengeneza vitambulisho ambavyo ni muhimu sana kuwa navyo.

Pia napenda kuwasisitiza kuwa wale wote wenye matatizo ya R.P (Residential Permit) na VISA tafadhali julisha uongozi wa TASABA ili tuweze kuwasaidia mapema kabla mambo hayajawa magumu zaidi.. Pia ni muhimu sana kuzingatia sheria na kanuni zote za uhamiaji ili kuepuka matatizo kama hayo. Wengi wenu mmeshashudia baadhi ya wenzetu wanavyopata matatizo makubwa juu ya mambo hayo.

Ndugu wa Tanzania wenzangu tukumbe mila na utamaduni wetu ni Amani, Umoja na Mshikamano. Nawaomba sana tudumishe utamaduni wetu kwa kuishi kwa amani baina yetu na wenyeji wan nchi hii. Masuala ya ugomvi kati yetu sisi kwa sisi au na wenyeji wetu hayatujengi zaidi ya kutupa sifa mbaya ambayo hapo baadae itatufanya tuishi katika wakati mgumu na inaweza kuwapa wakati mgumu wenzetu watakao kuwa wanahitaji kuja kusoma India siku zijazo. Naomba tufanye starehe za kiasi na za Amani. Tunaelekea kufunga mwaka kwa wale wote tuliobaki hapa Bangalore katika likizo hii naomba sana tuitumie vyema na ninategemea kuwa sitapata malalamiko ya ugomvi au tabia zozote zile amabzo si nzuri toka kwa jamii tunayoishi. Tukumbuke huku tuko ugenini na ni mbali na nyumbani hivyo tatizo lolote utakalolipata litasumbua mpaka wazazi nyumbani ambao wana kazi nyingi za kufanya .

Napenda kuwakumbusha tena kwa wale wote tunaotumia vyombo vya usafiri binafsi hasa pikipiki naomba tuwe makini sana. Najua kuna msemo usemao “AJALI HAINA KINGA” lakini tusichukulie msemo huu kama kigezo najua kuna ajali nyingine zinasababishwa na sisi wenyewe ama kwa kujiamini kuwa ni madereva wazuri au kwa kupenda sifa kutoka kwa wenzetu au kwa kushindwa kumiliki vyombo hivyo kutokana na ulevi. Tuna mifano mingi kutoka kwa wenzetu waliopata ajali hivyo basi nawaomba tuwe makini sana ili kuepuka tatizo hili najua wote ni watu wazima hivyo mtalizingatia hili kwa undani zaidi.

ndugu wa Tanzania wenzangu nazidi kuwaomba kutoa michango yenu ya halina Mali katika chama chetu ili kukijenga kiwe imara zaidi na cha manufaa kwa jamii nzima. Tukumbuke kuwa chama hiki ni chetu sote na kila mwanajumuiya ana haki sawa juu ya chama hiki katika kukijenga na kuleta maendeleo. Jukumu hili ni letu sote na si la viongozi wa chama au kundi Fulani. Napenda kuwa hakikishia kuwa TASABA hakifungani na kundi lolote lile kama uvumi uliopo. Uongozi wa TASABA ni uongozi wa jumuiya nzima na hauna kundi na wala hautakuja kuwa na kundi. Uongozi wa TASABA una wajibu wa kushirikiana na kila mwanajumuiya katika shida na raha hivyo basi hata siku moja hauta kuwa na manufaa katika kundi Fulani au mtu mojamoja uongozi huu ni wa kila mTanzania. Naomba tusiwe na mawzo potofu pia kuwakemea wale wote ambao wana mawazo potofu kama haya juu ya TASABA, kauli mbiu yetu ni “UMOJA NI NGUVU UTENGANO NI UDHAIFU” tushirikiane kwa pamoja na kudumisha amani, umoja na heshima miongoni mwetu na kwa jamii tunayoishi.

Napenda pia kuchukua fursa hii kuwapa pole wale wote waliofiwa na wazazi, na ndugu, kwa kipindi hiki. Mwenyezi Mungu awepe moyo wa uvumilivu na kuwaongoza vyema katika wakati huu mgumu mlikokuwa nao. Pia natoa pole kwa wale wote milopata matatizo ya kijamii, ugonjwa na ajali. TASABA ipo pamoja nanyi na itanedelea kushirikina nanyi bega kwa bega.

Nawatakia mapumziko mema, Mwenyezi Mungu awatangulie, awape afya njema, Hekima, Busara,Maarifa na mafanikio katika masomo yenu.

FIDELIS MARTINE MSOMEKELA
RAIS - TASABA

Wednesday, December 9, 2009

TANGAZO LA MICHEZO

FOR TANZANIAN FOOTBALL PLAYERS ,TUTAKUWA NA MAZOEZI YA PAMOJA UWANJA WA ACHARYA COLLEGE. SIKU YA JUMAMOSI TRH 12/12/09 KWA LENGO LA KUUNDA TANZANIA TEAM KWA AJILI YA MAANDALIZI YA MASHINDANO YA KIMATAIFA
KWA TAARIFA ZAIDI WASILIANA NA
WAZIRI WA MICHEZO
ABDALLAH"DULLA"
+919008772650

Tuesday, December 8, 2009

TASABA PRE INDEPENDENCE DAY(MATUKIO KATIKA PICHA)










Tarehe 5 decemba 2009 Tanzania Student Association of Bangalore(TASABA) wakishirikiana na watanzania wengine waishio Bangalore waliandaa shughuli ya Kusherekea uhuru wa Taifa letu la Tanzania.

YALIYOJIRI SEMINAR YA NOKIA FORUM 2010



Jana tarehe 7 decemba 2009 katika hoteli ya Taj Residency Mahtma Gandhi road hapa Bangalore,kulikua na semina kubwa ya watengenezaji wa simu wakubwa duniani wa kampuni ya Nokia baadhi ya wanafunzi wa kitanzania walipata bahati ya kuhudhuria semina hiyo wakiongozwa na msemaji mkuu wa Tasaba Mh.Jumanne Rajabu Mtambalike.
Mambo mengi yalizungumzwa kwenye semina hiyo, hasa katika ulimwengu wa sayansi na tekinolojia mabadiliko mbalimbali ya technolojia za matumizi ya simu zilizungumziwa na namna gani zitaweza kukuza uchumi wa nchi mbalimbali duniani. Semina ilifana na baadhi ya watu walipata fursa ya kujishindia Nokia N-97 pamoja na vitu mbalimbali vilitolewa na kampuni ya Nokia vikiwemo simu kwa washindi mbalimbali na kwa walihoudhuria walipata mabegi ya laptop,CD za software za mafundi wa nokia,pamoja na CD za graphics za kampuni ya Adobe Photoshop CS4,t-shirt,key olders na vitu vingine vingi ikiwa pamoja na kutambulika kama ni maofisa wapya wa Nokia duniani.
Mh Jumanne akilizungumzia hilo amesema hii ni changamoto kwa wanafunzi wote wakitanzania kujihusisha katika mambo kama haya kwa ajili ya kutengeneza msingi mzuri wa taaluma zao mbalimbali wanazosomea na kusisitiza hii ni nafasi wanayopata wanafunzi wanaosoma nje ya nchi hivyo waitumie vizuri.