Ads 468x60px

Pages

Wednesday, February 3, 2010

RIPOTI RASMI YA KIFO CHA BWANA “IMRAN MTUI”

Mnamo siku ya jumapili ya tarehe 31/01/2010, majira ya 9:30 alasiri uongozi wa wanafunzi waishio Bangalore India (TASABA) tulipokea taarifa ya kusikitisha kutoka kwa ndugu wa karibu wa marehemu kuwa kaka yetu mpendwa IMRAN MTUI kuwa tena duniani.
Mnamo majira ya saa tatu usiku mwenyekiti wa jumuiya ya wanafunzi waishio Bangalore (TASABA) Mh. Fidelis Msomekela aliwasiliana na ubalozi wa Tanzania New Delhi kuwafahamisha juu ya msiba wa mpendwa kaka yetu marehemu IMRAN MTUI.
Tarehe 1/02/2010 ofisi ya Ubalozi ilituma mwakilishi wake anayesimamia maswala ya wanafunzi India ili kusaidiana na serikali ya wanafunzi waishio Bangalore kujua chanzo zaidi juu ya kifo cha marehemu Imran Mtui.
Tarehe 2/01/2010, Mwakilishi wa ubalozi pamoja a mwenyekiti wa jumuiya ya wanafunzi Bangalore (TASABA) walifika katika kituo cha polisi kiitwacho ‘Cantonment Railway Police’ ili kupata ripoti kamili juu ya chanzo cha kifo cha marehu Imran Mtui. Ripoti ya polisi ilieleza kuwa mnamo majira ya saa 3:35 asubuhi mkaguzi wa reli alitoa taarifa kwa msismamizi mkuu wa reli kuwa ameona mwili wa marehemu IMRAN MTUI pembeni ya reli K.M No. 339/700-800 karibu na KRISHNARAJAPURAM LOCO SHED (MAHADEVAPUR, BANGALORE).
Taarifa za awali za polisi zinaeleza kuwa chanzo cha kifo cha marehemu Imran Mtui ni Ajali ya kawaida, uchunguzi zaidi unaendelea ili kujua chanzo kamili cha kifo cha ndugu yetu marehemu IMRAN MTUI.
Taratibu zote za kusafirisha mwili wa marehemu IMRAN MTUI zimekamilika, kesho (3/01/2010) majira ya jioni, mwili wa marehemu IMRAN MTUI utasafirishwa kuelekea nyumbani Tanzania kupitia kampuni la shirika la ndege la Emirates mpaka Dar es Salaam na baadae kusfirishwa kuelekea Killimanjaro kwa mazishi.
Uongozi wa Jumuiya ya wanafunzi waishio Bangalore (TASABA) unatoa shukrani za dhati kwa ubalozi wa Tanzania New Delhi kwa ushirikiano na msaada mkubwa walioutoa ili kufanikisha taratibu zote za kisheria na kutoa usafiri wa kumsafirisha ndugu yetu maarehemu IMRAN MTUI mpaka nyumbani kwao Kilimanjaro. Pia uongozi wa Jumuiya ya wanafunzi waishio Bangalore (TASABA), unatoa shukrani za dhati kwa wale wote walioungana na familia ya ndugu yetu mpendwa marehemu IMRAN MTUI kwa hali na mali.
Jumuiya ya wanafunzi waishio Bangalore (TASABA),unaomba wanajumuiya wote kuwa watulivu na kuacha kutoa habari za kizushi juu ya kifo cha marehemu IMRAN MTUI kwa kuwa uchunguzi zaidi bado unaendelea na mpaka sasa hakuna mtuhumiwa yoyote Yule anaye shutumiwa au kushikiliwa na polisi juu ya kifo hicho.
Uongozi wa wanafunzi waishio Bangalore (TASABA) unatoa pole kwa familia ya marehemu IMRAN MTUI. Mungu aiweke mahali pema peponi roho ya ndugu yetu mpendwa marehemu IMRAN MTUI. Amin
Fidelis Msomekela
President – TASABA
03/02/2010

4 comments:

KAONEKA said...

KWA MASIKITIKO MAKUBWA WANAFUNZI WATANZANIA NCHINI ALGERIA (ATSA) WANAINGANA NA WANAFUNZI WOTE WATANZANIA DUNIANI KOTE KUOMBOLEZA KIFO CHA MWANAFUNZI MWENZETU BWANA "IMRANI MTUI"
MUNGU AILAZE ROHO YA MAREHEMU MAHALI PEMA PEPONI AMIN

KWA MAELEZO ZAIDI YA WANAFUNZI NCHINI ALGERIA TEMBELEA TOVUTI YAO HAPA
www.atsa-tz.ning.com

Anonymous said...

tutakukumbuka kaka daima rest in peace

Anonymous said...

kama ni kifo cha kawaida Mungu ashukuriwe, kama sio cha kawaida Mungu huyo huyo atajibu!!!
Mungu aiweke roho yake mahali pema peponi,

ray05 said...

Kwanza nawapa pole ndugu wa marehemu IMRAN MTUI na waTanzania wote kwa ujumla.

Hakuna aliyepanga hili bali ni Mungu pekee hivyo tuendelee kumuomba yeye ili atusaidie kwani hatujui siku wala saa.tunawaomba ndugu wa marehemu na wanafunzi waTanzania wanaosoma India wasione kama wapo wenyewe kwenye msiba huu bali wapo pamoja na dunia nzima katika hili.tumesikitika sana na tunasubiri hiyo ripoti ya polisi ili tujue nini chanzo hasa cha kifo cha Imran.

Mungu ailaze pema roho ya marehemu,YEYE AMETANGULIA NASI TUTAFUATA...Amen!!

Post a Comment