Ads 468x60px

Pages

Monday, March 22, 2010

TANGAZO

Kuhusiana na matatizo yaliyotokea hivi karibuni maeneo ya Hennur uongozi wa TASABA chini ya Rais Fidelis Msomekela ulifikia makubaliano pamoja na jeshi la polisi la Bangalore pamoja na mwakilishi wa ubalozi wetu Mh.Amon Mwamunenge kuhusiana na kuongeza ulinzi kwa wanafunzi wakitanzania waishio Bangalore.
Kutokana na hilo uongozi wa TASABA unasisitiza wanafunzi ambao hawajajiandikisha majina yao na kuchukua kitambulisho cha uanachama cha TASABA, watakua kwenye wakati mgumu wakipatwa na matatizo kwa sababu uongozi wa TASABA hauna taarifa zao rasmi kuhusu maeneo wanayokaa na namna ya kuwafikia. Hivyo watanzania wote waishio Bangalore wameombwa kujiandikisha na kuchukua fomu haraka iwezekanavyo kwa viongozi wao wa maeneo.Hii ni kwa wote ambao hawana kitambulisho cha TASABA mpaka hivi sasa.
TASABA SPOKESMAN
JUMANNE MTAMBALIKE

0 comments:

Post a Comment